PUFF MINISTRY kama tulivyokwambia kuwa puff tutakuwa na tamasha tarehe ishirini na nne. PUFF tuliandaa tamasha kubwa lililofanyika katika ukumbi wa viziwi mjini Njombe lililo kuwa na wageni mbalimbali na wanakwaya kutoka sehemu mbalimbali,pia kulikuwa na uzinduzi wa album ya dada yetu Adefrida Mlowe aliye zindua album yake iliyotoka kwa jina la safari ya mbinguni. ni nyimbo zilizo pendwa na watu sana ewe msomaji wetu endapo utaiona na kuisikiliza utatupa maoni yako katika mtandao au kupiga simu no 0756241281/0759700254.bila kusahau PUFF RECORDS tuliandaa shindano kubwa la kwaya mbalimbali lilikuwa ni shindano lililo burudisha sana na kama ada katika furaha hapakosi changamoto tulipata changamoto nyingi. ila tuliweza kupata washindi bora kabisa kwaya ya Hossiana inayotokea Ramadhani Njombe katika kanisa la K.K.K.T Yeriko ndio ilituongozea ushindi ilishika nafasi ya kwanza kwa 81% na ilipewa furusa kubwa na studio zetu za puff ofa hiyo ni ku record albam nzima ya audio bila malipo, na mshindi wa pili alipewa fursa ya ku record vocal bila malipo yoyote hii ni zawadi nono kutoka PUFF RECORDS.pia mgeni rasmi alitoa fursa kubwa kwa dada Adefrida Mlowa ofa hiyo ni asilimia ishirini na tano ya kurecod video yake. tunapenda kukukalibisha katika tamasha lijalo litakalo andaliwa na PUFF
ungana nasi katika huduma zetu kupitia BLOG hii
.
KWA MAONI na USHAURI PIGA NAMBA HIZO HAPO JUU
PUFF INACHUKUA MUDA HUU KUKUSHUKURU MSOMAJI
WETU PIA INAPENDA UTUUNGE MKONO.
ASANTE & KARIBU